Quantcast
Channel: BongoClan Tanzania™
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3623

AY AKANA KUA YEYE NDO HUA ANAMWANDIKIA NYIMBO MSANII JAGUAR, HIKI NDO ALICHOKISEMA HAPA

$
0
0


Nchini Kenya kumekuepo na minongono kua msanii AY amekua akimwandikia nyimbo Jaguar kutoka Kenya. Hii imetokana na ukaribu mkubwa walionao wasanii hao. Kwa mujibu wa chanzo chetu nchini Kenya inasemekana kuna baadhi ya watu wanaamini kua kuna ukweli katika hilo.

Baada ya kuzagaa kwa maneno hayo AY ameamua kuvunja ukimya na kufunguka kua hajawahi kumwandikia wimbo hata mmoja Jaguar. AY aliendelea kusema “ Jaguar ni mmoja kati ya marafiki zangu wakubwa. Nimefanya nae kazi na bado ninaendelea kufanya nae kazi, na hakuna ukweli wowote kua ninamwandikiaga nyimbo zake. Jaguar ni mtu anayejitegemea, na amekua katika fani ya mziki kwa mda mrefu jambo linalomfanya kua na uzoefu mkubwa katika kile anachokifanya. Hata katika kolabo niliyofanya nae nimetoa mbali aliandika mistari yake yeye mwenyewe name nikaandika yangu”


Viewing all articles
Browse latest Browse all 3623

Trending Articles