Quantcast
Channel: BongoClan Tanzania™
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3623

NGASSA APELEKA MPIRA WA HAT TRICK ALIOPEWA TAIFA KWA WEMA SEPETU, SOMA ALICHOKISEMA HAPA

$
0
0
WEMA
“Diamond ni rafiki yangu, lakini mpira huu nitampelekea Wema kwa kuwa ni shemeji yangu na tunaheshimiana sana,” alisema Ngassa na kuongeza:
Mrisho Ngassa wa Yanga, jana alifanikiwa kufunga mabao matatu ‘hat trick’ katika mechi dhidi ya JKT Ruvu, lakini ametoa kali kwa kusema kuwa mpira aliokabidhiwa kwa kufunga mabao hayo, anaupeleka kwa shemeji yake, Wema Sepetu.
Akizungumza baada ya mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara iliyomalizika kwa timu yake kupata ushindi wa mabao 5-1, Ngassa huku akionyesha kuwa na furaha, alisema kuwa mpira huo umeongeza hamasa kwa timu yake, lakini moja kwa moja atampelekea Wema ambaye ni mpenzi wa mwanamuziki Diamond.
“Mashabiki hawatakiwi kukata tamaa na timu yetu, sisi tutapigana mpaka dakika ya mwisho ili kuhakikisha tunashinda mechi zote. Wakati mwingine tunashindwa kucheza vizuri mikoani kwa kuwa viwanja vinakuwa havina ubora mzuri.” 
Yanga imepata ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya JKT Ruvu na hivyo kuamsha mbio za ubingwa dhidi ya Azam ambao ndiyo vinara wa Ligi Kuu Bara, lakini kipa Juma Kaseja na mshambuliaji raia wa Uganda, Emmanuel Okwi hawakuwepo kwenye kikosi kilichoanza wala kwenye benchi.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3623

Trending Articles