Quantcast
Channel: BongoClan Tanzania™
Viewing all 3623 articles
Browse latest View live

Picha: Ni Wema Sepetu na Ommy Dimpoz wakipeana 'Kiss' mdomoni huku wakiwa kwenye hali ya mahaba mazito!

$
0
0
Hatimaye ile project iliyokuwa inasubiriwa kwa muda mrefu sasa kesho ndio siku rasmini itakayo toka. Ambapo Ommy Dimpoz ame share picha ikimuonyesha akiwa na Wema Sepetu kitandani kama wana peana kiss mdomoni nakuandika "Tomorrow...Saa 4 Asubuhi kwenye TV na Radio zote Ndani na Nje ya Nchi....#WANJERA"
Lakini pia hata Wema Sepetu ame share picha ikionyesha wamesimama na Ommy Dimpoz wakiwa kwenye hali ya kimahaba na kuandika "Stay tuned... tomorrow @10 am... Kweny radio na Tv zote....(Local & International) I cant wait... Finally...!!Wanjera..!!!".

Linex Feat. Diamond Platnumz - Salima (Official Video)

New Video : Ibrah ft Mubanda Real Love Official Music Video full HD

Mwanamke Aliye Mrekodi Video Ya UCHI Mtangazaji wa Runinga ya TV1, Ezden Akamatwa na Jeshi La Polisi

$
0
0

JESHI la polisi jijini Dar limemkamata binti anayefahamika kwa jina la Moza kwa kosa la kudaiwa kumdhalilisha Mtangazaji wa Runinga ya TV1, Ezden Jumanne ambapo anatarajiwa kuburuzwa mahakamani muda wowote baada ya uchunguzi kukamilika.

Moza ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtangazaji huyo kisha kuachwa, anadaiwa kumrekodi video ya utupu Ezden kipindi walipokuwa kwenye uhusiano mzuri kisha kuisambaza mitandaoni walipogombana.
 
Chanzo makini kimedai kuwa, Moza alikamatwa na kuwekwa mahabusu katika Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar kufuatia msako mdogo uliofanywa na polisi saa chache baada ya mrembo huyo kuvujisha video hiyo.
 
“Wameshamtaiti pale Oysterbay, wanakamilisha tu taratibu za ushahidi kisha anaburuzwa mahakamani muda wowote kuanzia sasa,” kilisema chanzo chetu, juzi Jumatano. 
 

Moza amedaiwa kuiachia video hiyo mapema wiki hii kutokana na chuki za kuona Ezden ana mwanamke mwingine hivyo akaona akivujisha video hiyo atakuwa amemkomoa mtangazaji huyo kijana aliyewahi kuwa mume wa Mtangazaji Khadija Shaibu ‘Dida’.

Akizungumzia sakata hilo, Ezden alisema yeye ni mtu anayejiheshimu, anajitambua hivyo kitendo cha mwanamke huyo kumrekodi video hiyo hakikuwa cha kiungwana.
 
“Hakunitendea haki, Nimeshalifikisha suala hili polisi, taratibu za kipolisi zikikamilika anaburuzwa mahakamani,” alisema Edzen.

New Video : Ommy Dimpoz - Wanjera. Ndani yumo Wema Sepetu na Idriss mshindi wa BBA

Sikiliza na Download Ommy Dimpoz - Wanjera

Masanja awashusha Profesa Jay na Jaydee, sasa awa msanii wa pili kwa utajiri Tanzania.

$
0
0
UTAJIRI wa komediani maarufu Bongo, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ ni kufuru! Tena unatisha na sasa anaonekana kuwa miongoni mwa wasanii wACanaomiliki fedha na mali nyingi Bongo, Risasi Mchanganyiko linakupa zaidi.

HABARI MEZANI
Awali, habari kuhusu utajiri wa Masanja ilitua mezani mwa gazeti hili kama kidokezo, hapo mwandishi wetu akaingia mzigoni na kuanza kuchunguza kwa kina mali anazomiliki msanii huyo na kugundua kuwa ni kati ya mastaa mabilionea Bongo.
“Masanja sio yule tena. Ana mpunga (fedha) mrefu sana. Hakuna msanii wa maigizo Bongo anayeweza kumfikia kwa sasa. Hao wengine ni mbwembwe tu, lakini pesa imelala kwa Masanja,” kilipasha chanzo chetu.

Kikaongeza: “Kwanza ana ghorofa lipo Tabata, hapo ndipo anapoishi. Pia ana magari kibao ya kifahari, mashamba ya mpunga na Kampuni ya OK Security inayolinda sehemu mbalimbali zikiwemo taasisi nyeti nchini.


“Ni msanii gani mwenye kampuni kubwa kama ya Masanja? Wengi wanaishia kudai wanatayarisha filamu ambazo hata matunda yake hayaonekani.”

RISASI MZIGONI
Mdogomdogo, Risasi Mchanganyiko likajitupa mtaani kuchimba kuhusu madai hayo ambayo awali liliyatilia shaka kama si wasiwasi.
Uchunguzi wetu ulibaini ukweli wa mali za msanii huyo na mambo mengine mengi yanayoingia kama vyanzo vya mapato yake.

MAGARI SITA
Ilibainika kuwa, Masanja anamiliki magari sita, yakiwemo ya kifahari. Baadhi ya magari hayo ni Toyota Land Cruiser V8, Nissan Hardboad na Toyota Verossa.
http://1.bp.blogspot.com/-qf3f5-BRw6s/VCknFidh56I/AAAAAAAAp1M/BjfmWcNuL4o/s640/mkandamizaji.jpg

NYUMBA TATU BONGO
Pia, mkali huyo wa kuvunja mbavu, anamiliki nyumba tatu za maana jijini Dar es Salaam, moja ni ghorofa ipo Tabata, nyingine Kigamboni na nyingine haifahamiki eneo rasmi ilipo.
Hata hivyo, imebainika kuwa mbali na mijengo yake hiyo iliyopo jijini Dar, nyumbani kwao Mbarali, Mbeya ana mjengo wa maana.
http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2013/06/957235f6cfb811e2855722000aa800e1_7.jpg

MASHAMBA KIBAO
Msanii huyo hayupo nyuma kwenye kilimo, ana mashamba kadhaa Kigamboni jijini Dar es Salaam lakini linalotia fora ni lile lililopo Mbarali lenye ukubwa wa hekari 50 ambalo analima mpunga.

http://3.bp.blogspot.com/-v-HlI8AT0Wc/UdBPG8PTk7I/AAAAAAAAAW0/Pb5oMSZyVM8/s640/mbarali.jpg
NI MSANII WAMAIGIZO TAJIRI ZAIDI?
Kwa utajiri huo, ipo minong’ono kuwa, nyota huyo anaweza kuwa kwenye namba za juu za wasanii wa maigizo wenye mkwanja mrefu.
Wengine wanaotajwa kwenye orodha ya waigizaji matajiri Bongo ni Husna Posh ‘Dotnata’, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ na Amri Athumani ‘Mzee Majuto’.

]MATAJIRI BONGO FLEVA
Katika muziki wa Bongo Fleva, wasanii wanaoaminika wana utajiri mkubwa zaidi ni Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Joseph Haule ‘Profesa Jay’.
Wasanii hao wanamiliki mijengo ya maana, achilia mbali magari ya kifahari na miradi kadhaa.
http://2.bp.blogspot.com/-u1bQLMgIYd0/UbkRx2MwLOI/AAAAAAAAJrQ/s7INkdZJiHA/s1600/10.jpg
MASWALI KUHUSU MASANJA
Utajiri wa Masanja umeonekana kuibuka ghafla huku vyanzo vyake vya kumwingizia kipato vikijulikana ni sanaa ya uigizaji, muziki na huduma ya uchungaji.

Je, kwa uigizaji tu katika Kundi la Orijino Komedi ‘OK’ ndiko alikopata mkwanja huo na kuanzisha miradi hiyo mikubwa?

Kama ndiyo, kwa nini memba wenzake ndani ya kundi hilo hawana maendeleo makubwa kama yeye?
http://1.bp.blogspot.com/-7Y0LuOkVCGk/Uwv3ePqchBI/AAAAAAAFPWM/A_P74vLntkk/s1600/IMG_1621.jpg
Kazi nyingine ya Masanja ni muziki wa Injili ambapo kwa sasa albamu yake ya Hakuna Jipya iko sokoni. Je, albamu hiyo na shoo anazofanya zinaweza kuwa chanzo cha utajiri huo?

Lakini pia Masanja ni mchungaji ambaye anahudumu katika Kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT) ‘Mito ya Baraka’ lilicho chini ya Askofu Bruno Mwakiborwa. Je, mshahara anaoupata kutokana na huduma hiyo unaweza kuwa chanzo cha mapato yake?

Risasi Mchanganyiko halikutaka kupasua kichwa, juzi lilimsaka Masanja kwa simu na kumhoji juu ya mali zake ambapo kwanza alithibitisha kweli anamiliki mali hizo na nyingine ambazo hakupenda kuzitaja.

“Ni kweli nina nyumba tatu hapa mjini, kampuni ya ulinzi na mashamba ya mpunga eka 50 nyumbani Mbarali, Mbeya. Kuhusu magari pia ni kweli kabisa. Mimi ni mtumishi sitakiwi kusema uongo,” alisema Masanja.

RISASI: Lakini mbona utajiri wako umekuwa wa haraka sana mtumishi, vipi vyanzo vya mapato yako?

MASANJA: Orijino Komedi ndiyo chanzo cha vyote... pale ndipo kwenye koki.

RISASI: Kuchekesha tu kaka? Au kwenye muziki wa Injili pia kunalipa?

MASANJA: Injili na uchungaji ninaotumika kanisani ni huduma kaka, sitegemei mapato kutoka huko. Nipo kwa ajili ya kulisha kondoo wa Bwana.

RISASI: Wasanii wenzako wa Orijino Komedi wanachukuaje mafanikio yako?

MASANJA: Wanafurahia, wananiunga mkono maana ni sehemu ya mafanikio yao pia. Sisi tunaishi kama ndugu. Kwa hiyo kuna baadhi ya aidia ni zao, hivyo wanajivunia sana mafanikio yangu.

Tuituitui! Simu ikakatika!

Picha 5 za jumba la kifahari analoishi Spika wa Bunge, ni la thamani ya bilioni 1 na nusu.

$
0
0

Hatimaye Spika wa Bunge la Tanzania pale Dodoma atakuwa na makazi rasmi baada ya ujenzi wa nyumba ya Spika kukamilika na makabidhiano kufanyika. Nyumba hiyo ambayo ipo maeneo ya

Uzunguni nje kidogo ya Dodoma mjini imegharimu takribani Tshs 1.5 

Billion na imejengwa na kampuni ya Pacha Building Construction Company.
 Hii inakuwa nyumba ya kwanza rasmi ya Spika kwani hapo awali hapakuwahi kuwa na nyumba rasmi ya Spika.

Picture
Picture
Mlango wa mbele
Picture
Upande wa nyuma wa jengo
Picture
Ngazi ndani ya jengo ambalo lina vyumba vinne vya kulala, sehemu ya mapumziko, sehemu ya chakula, maktaba na jiko (picha: Prosper Minja)

New Video : Jux - Nikuite Nani [Official Video]

Penny Adaiwa Kunywa Sumu Kisa Kunyang'anywa Bwana na Shosti Yake

$
0
0
MTANGAZAJI maarufu Bongo na aliyekuwa mpenzi wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Penniel Mungilwa ‘Penny’ amedaiwa kunywa sumu kufuatia kunyang’anywa bwana na shosti yake aliyefahamika kwa jina la Diana.

Kwa mujibu wa chanzo, Penny na Diana walikuwa marafiki lakini wakatofautiana baada ya Diana kumteka akili mwanaume wa rafiki yake huyo na kumkoleza mapenzi hadi kufikia hatua ya kumtangazia ndoa.

“Diana kampagawisha mwanaume wa watu, jamaa akatangaza ndoa na hivi ninavyokwambia siku siyo nyingi Diana anaolewa hicho ndicho kikasababisha Penny apandwe na presha hadi kufikia hatua ya kunywa sumu, alikimbizwa hospitali, akalazwa lakini sasa ametoka anaendelea vizuri,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kuzinyaka habari hizo, mwanahabari wetu alimtafuta Penny ili kujua anazungumziaje habari hizo za kunywa sumu hadi kulazwa hospitali ambapo alikanusha madai hayo.
“Sijanywa sumu, suala la mimi kulazwa huwa linatokea sababu nasumbuliwa na pumu mara kwa mara,” alisema Penny.

Chanzo:Globalpublishers

Mambo yameiva kwa Wema, sasa kuolewa na aliyekua mume wa Zari.

$
0
0
http://api.ning.com/files/1R1gqINM7bxlzUrR3WwslSL-E8TbeHC1JSrbNDKpWvHYhQ*hGsLGGlY*A*9JAwMlII53Jl2VqX4dOUldYfKBDNEL-SD2so7n/wemadivorce.jpg
Stori: MUSA MATEJA/Risasi wa Global Publisher
MAMBO hadharani! Supastaa wa Bongo, Wema Sepetu ‘madam’ ameanika siri zilizojificha nyuma ya pazia kati yake na aliyekuwa mume wa mwanamuziki nyota wa Uganda, Zarina Hassan ‘Zari’, Ivan Semwanga, kuwa anataka kumuoa, Risasi Jumamosi lina full stori.
 
.WALIANZIA KUKUTANA SAUZ
Katika mazungumzo yake exclusive na mwanahabari wetu juzi jijini Dar, Wema alianza kwa kuweka bayana kwamba, mawasiliano yake na Ivan yalianzia nchini Afrika Kusini wakati alipokwenda kikazi, Februari, mwaka huu.
“Nilikwenda na Ommy Dimpoz (Faraj Nyembo). Tulikuwa na project yake lakini tulipokuwa kule, Ivan na marafiki zake walisikia kuwa mimi nipo, wakatuomba sana kupitia kwa wenyeji wetu kuwa wanataka kutuona na kutoka nao out pamoja.”

ALIBANA, AKALEGEZA
“Mimi nilikuwa bize sana na kazi zangu, awali niliwaambia kuwa hatutaweza lakini baadaye walitubahatisha klabu, wakaomba kukaa na sisi, mwishoni ilibidi tuwakubalie lakini kwa masharti ya kuwa wasije wakatuzushia lolote.
“Tulikubali, wakaja, tukakaa nao meza moja, tukabadilishana mawasiliano kama marafiki. Lakini baadaye tukaona wanaongezeka, sikupenda vurugu ya watu wengi, mimi na Ommy tukaamua kuondoka zetu,” alisema Wema.

IVAN AANZA ‘KUIMBISHA’
Akizidi kumwaga siri zake na mwanaume huyo, Wema alisema baada ya yeye kumaliza project yake nchini humo, alirejea Bongo na ndipo Ivan alipozidisha ufundi wa kumuomba urafiki wa kimapenzi huku akimuahidi mambo mengi ya muhimu.
Msikie Wema: “Baada ya hapo tulikuwa tunawasiliana na Ivan, lakini kadiri siku zilivyokuwa zikisonga mbele, nikaona mwenzangu anaanza kunitongoza, tena akawa anaendelea kila siku licha ya mimi kutomkubalia.”

AHADI  NI  MAGARI, NYUMBA
Wema alizidi kutiririka kuwa, hadi sasa (mapema wiki hii), Ivan hajakata tamaa, amekuwa akiendelea kumtongoza na kumuahidi ahadi mbalimbali.
Endapo atamkubalia na kuwa baby wake, basi atampa nyumba ya kifahari na magari ya kisasa (awe kama Zari).
Wema anakiri mwenyewe: “Alianza kuniahidi maisha mazuri, nyumba, magari na hata kunioa lakini kimsingi sijamkubalia kwani sijamwamini kama ana mapenzi ya dhati. Nahisi kuna kitu nyuma yake kinamsukuma kufanya hivyo.”

ATAKIWA KUTOICHEZEA BAHATI
Kwa mujibu wa chanzo makini, kuna uwezekano mkubwa Wema akaingia kwenye himaya ya Ivan kutokana na ushawishi wake mkubwa anaoufanya kwa madam huyo, hivyo akawa tajiri mkubwa.
“Wema kwa sasa hatakiwi kuichezea bahati kwani Ivan ni mtu anayejiheshimu. Ana biashara zake kubwakubwa, hivyo suala la fedha za maisha hazimpigi chenga,” kilisema chanzo hicho.

WEMA KUWA KAMA MCHARO?
Akizungumzia suala hilo, rafiki wa karibu wa Wema ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini, alisema licha ya Wema kutokubali ombi la Ivan lakini anaamini siku si nyingi atakubali na atakuwa vizuri kiuchumi kuliko alivyo sasa.
“Jamaa yupo serious na ndoa, Wema atakubali tu na ndoa itafungwa. Mtoto wa kike sasa atakuwa si wa magari ya kawaida, full kubadilisha, atakuwa mtamu kama mcharo,” alisema rafiki huyo.

KINACHOMPA WASIWASI WEMA
Rafiki huyo aliendelea kusema kuwa, Wema ana wasiwasi kwamba, mapenzi ya Ivan kwake ni kwa ajili ya kulipa kisasi kwa sababu ya Diamond (aliyekuwa mpenzi wa Wema) sasa yuko na Zari (aliyekuwa mke wa Ivan).
“Kwa hiyo Wema ana wasiwasi kwamba, siku akimkubalia tu Ivan akapiga naye ngwara, biashara itakuwa imeishia hapo kwani nia ya kisasi ya mwanaume huyo itakuwa imekamilika,” alisema rafiki huyo.

Wimbo Mpya wa Ommy Dimpoz Wapondwa ila Video Yasifiwa

$
0
0
Baada ya Video mpya ya Ommy Dimpoz Kutoka Jana Baadhi ya Watu wakiwemo bloggers Maarufu kama U-turn Wameendeleza kuponda tunzi na melody za nyimbo zinazotolewa hivi sasa hasa kutoka kwa wanamuziki wakubwa ..Tukija kwenye hii nyimbo mpya ya Ommy Dimpoz ya Wanjera Wengi wamesema hakuna jipya kwenye wimbo na mashairi ila Video imetokea bomba hasa ukichukulia na uwepo wa Wema Sepetu ndani yake ... ...Bado msisitizo wa wasanii wakubwa kukubali kutungiwa nyimbo unawekwa ili kupata ladha tofauti ...Je wewe una maoni gani??

Snura adaiwa kupora mume wa msanii mwenzake kutoka Bongo Movie, aliyeibiwa afunguka.

$
0
0
Staa wa muziki wa mduara, Snura Mushi ameingia katika tuhuma nzito akidaiwa kutoka kimapenzi na mume wa rafiki yake Halima Yahya ‘Davina’.
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, kwa kipindi kirefu, Snura amekuwa akionekana nyakati za usiku akiwa na mume wa Davina, wakati mwingine mwanaume huyo anaenda nyumbani kwa Snura au wawili hao kuzungumza kwa muda mrefu ndani ya gari la mwanaume huyo.
http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2013/11/snura-234.jpgStaa wa sinema na muziki wa Bongo Fleva, Snura Mushi.
“Yaani mastaa wa Bongo bwana, wanapenda sana kuchukuliana mabwana. Huyu Snura anatoka na mume wa mwenzake. Mume wa Davina huwa anakuja nyumbani kwa Snura mara kwa mara hasa nyakati za usiku.
“Wakati mwingine anakuja na gari na kupaki jirani na nyumbani kwa Snura kisha wanakaa kwenye gari kwa saa kibao. Snura anamzunguka rafiki yake,  fuatilieni mtaujua ukweli,” kilisema chanzo chetu.
Baada ya kuunyaka ubuyu huo, Ijumaa Wikienda liliamua kuingia mzigoni kwa kumsaka Snura na alipopatikana, akasomewa tuhuma zake ambapo katika hali ya kushangaza, msanii huyo, alimwaga chozi.

Staawa Bongo Movies, Halima Yahya ‘Davina’.
Alipomaliza kulia, Snura alianza kufunguka ukweli wa kisa hicho ambapo alikiri kuwa ni kweli mume wa Davina alikuwa akienda nyumbani kwake mara kwa mara lakini ilikuwa ni kipindi ambacho Davina na mwanaume huyo walikuwa wametibuana kiasi cha msanii huyo kufungasha virago vyake na kutokomea kusikojulikana.
“Mimi nilikuwa nahangaika kuwapatanisha kwa sababu walikuwa kwenye mgogoro mkubwa, mumewe akawa ananiomba nimsaidie kumbembeleza Davina arudi wayazungumze na kumaliza matatizo yao ili kuokoa ndoa yao isivunjike.
Ijumaa Wikienda halikuishia hapo, lilimtafuta pia Davina ili kujua kwa upande wake analizungumziaje sakata hilo ambapo msanii huyo alitema nyongo. Hebu msikie:
“Watu wengine hawana kabisa kazi za kufanya, yaani walikuwa wanataka kunigombanisha na shosti wangu lakini wameshindwa. Ni kweli na mimi niliwahi kuletewa taarifa kwamba mume wangu anaonekana nyumbani kwa Snura usiku lakini ilikuwa ni kipindi ambacho nilikuwa kwenye matatizo na mume wangu.
“Kiukweli Snura hawezi kufanya hivyo kwa sababu yeye ndiye aliyepigania ndoa yangu isivunjike. Isitoshe sisi tunaishi kama ndugu, watoto wangu huwa wanaenda kushinda kwake na wakati mwingine huwa namtuma mume wangu akawachukue kwa hiyo hata kama wanamuona kwake, siyo kwa nia mbaya, watu aache uchonganishi,” alisema Davina.

Diamond Anusirika Kukatwa Mguu...Ugonjwa Unaomsumbua ni Hatari Sana..Afanyiwa Upasuaji..Video

$
0
0
Mwanamuziki Diamond Platnumz Amejikuta katika wakati mgumu Baada ya Tatizo la Mguu lilikuwa likimsumbua kwa miaka miwili kufikia hatua mpaka kufanyiwa upasuaji kuokoa mguu wake usikatwe..Diamond alipelekwa Hospitali ya TMJ baada ya maumivu kuzidi na baada ya kufanyiwa uchunguzi aligundulika na Ugongwa unaitwa FOOT CORN ama Kisahani kwenye Goti ..Ambapo Daktari alisema ni Ugonjwa mbaya sana ambao usipotibiwa haraka hulazika mgonjwa kukatwa Mguu..Diamond amefanyiwa upasuaji na kuondoa Tatizo hilo katika Mguu wake ..

Angalia Video Hapa chini Akiwa Katika Chumba cha Upasuaji:

Mkazi wa Korogwe, Tanga aibuka mshindi wa mtoko wa Mbugani kwenye fainali ya kampeni “Tutoke na Serengeti”

$
0
0
4
Meneja chapa wa bia ya Serengeti Premium, Bw.Rugambo Rodney (wa pili kulia), akionyesha namba ya simu ya mshindi wa mwisho wa shindano la Tutoke na Serengeti, ambapo Bw. Robert Gabriel mkazi wa Korogwe, Tanga aliibuka mshindi.Msimamizi toka PWC, Golder Kamuzora na (wa pili kulia), Afisa mwandamizi toka bodi ya michezo ya kubahatisha,Bw. Jehud Ngolo (wa kwanza kushoto) Afisa Mauzo toka SBL, Anitha Moshi, (wa kwanza kulia). Droo hiyo iliyofanyika katika baa ya Hongera jijini Dar es salaam.
5
Mmoja wa washiriki wa droo ya mwisho ya “Tutoke na Serengeti,” Morris Maro wa pili toka kulia akibonyeza kitufe cha laptop kuchezesha droo hiyo wakati wa kumtafuta mshindi wa mwisho wa “Mtoko wa mbugani” katika kampeni ya Tutoke na Serengeti. Droo hiyo ilifanyika Hongera baa iliyopo Kijitonyama jijini Dar es salaam amapo Bw. Robert Gabriel mkazi wa Korogwe,Tanga aliibuka mshindi. Kwenye picha ni Meneja chapa bia ya Serengeti premium Bw. Rugambo Rodney (wa pili  kushoto), Afisa mwandamizi toka bodi ya michezo ya kubahatisha, Jehud Ngolo (wa kwanza kushoto), na Getrud Mzava*mteja) aliyeitwa kushuhudia, droo hiyo ikichezeshwa kwa haki ndani ya ukumbi wa Hongera baa-Kijitonyama jijini Dar es salaam.
6
Mmoja wa wateja wa Serengeti Premium Lager, Getrud Mzava ,akitaja namba za simu za mshindi wa mwisho katika droo ya Tutoke na Serengeti wakati wa kumtafuta mshindi wa mwisho wa Mtoko wa mbugani, ambapo mkazi wa Korogwe,Tanga,Bw.Robert Gabriel aliibuka mshindi wa Mtoko wa Mbugani. Droo hiyo ilichezeshwa ndani ya ukumbi wa Hongera-Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
7
Meneja Bia chapa ya Serengeti Premium Lager, Bw. Rugambo Rodney (wa pili kushoto), akiongea kwa njia ya simu na mshindi wa mtoko wa mbugani, Bw. Robert Gabriel mkazi wa Korogwe-Tanga, baada ya kuibuka mshindi wa mwisho wa shindano la Tutoke na Serengeti katika droo iliyochezeshwa ndani ya ukumbi wa Hongera baa-Kijitonyama jijini Dar es salaam.Kulia ni Afisa mwandamizi toka Bodi ya michezo ya kubahatisha, Jehud Ngolo.
8
Meneja chapa wa bia ya Serengeti Premium Bw. Rugambo Rodney, (kushoto) akiongea kwa njia ya Simu na mshindi wa “Mtoko wa mbugani” Robert Gabriel mkazi wa Korogwe-Tanga, baada ya kuibuka mshindi wa mwisho wa shindano la Tutoke na Serengeti. Droo hiyo ilichezeshwa ndani ya ukumbi wa Hongera Baa-Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
10
  Wasanii toka SBL wakikonga nyoyo za  washiriki wa Droo ya Tutoke na Serengeti wakati wa kumtafuta mshindi wa mwisho wa “Mtoko wa Mbugani” ambapoBw.Robert Gabriel toka Korogwe-Tanga aliibuka mshindi wa droo hiyo iliyochezeshwa jana katika Baa ya Hongera iliyopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
2
Mmoja wa washindi wa shindano la Tutoke na Serengeti, Bw.Godfrey Mpiruka aliyeibuka na zawadi ya Limo Bajaji siku za nyuma akiteta jambo na afisa toka SBL wakati wa kuchezeshwa kwa droo ya mwisho ya shindano hilo, lililofanyika katika baa ya Hongera iliyopo-Kijitonyama jijini Dar es salaam.
Droo ya mwisho ya kampeni ya Tutoke na Serengeti imemshuhudia mkazi wa Korogwe Tanga Bw. Robert Gabriel Moriale akitangazwa mshindi katika fainali ya kampeni “Tutoke na Serengeti”. Fainali hiyo imefanyika katika ukumbi wa Baa ya Hongera iliyopo maeneo ya Kijitonyama-Dar es salaam karibu na chuo cha Ustawi wa jamii.
 Mshindi huyo alijipatia fursa ya kutembelea hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambapo ataongozana na mtu wake yeyote wa karibu kwa muda wa siku tatu huku SBL kupitia bia yake ya Serengeti Premium ndio itahusika kugharamia usafiri, chakula, malazi sambamba na fedha taslim za mshindi kujikimu pindi atakapokua safarini.
Akiongea kupitia njia ya simu mara baada ya kutangazwa mshindi wa mtoko wa mbugani, Bw.Robert  (49)alipokea taarifa hizo kwa furaha na alisikika akishangilia kwa kelele baada ya kuambiwa kwamba amejishindia “Mtoko wa Mbugani”.
Alipoulizwa kama alishawahi kushinda chochote kabla ya zawadi hiyo, Robert alijibu “Nimekuwa nikishiriki tangu mwanzo na nimepata bia za bure nyingi tu pamoja na pungozo la Tsh 300. Lakini hii ya leo kwa kweli sikuitarajia kabisa”
Akiongea wakati wa kufunga kampeni hiyo, Meneja chapa wa bia ya Serengeti Premium Lager , Bwana Rugambo Rodney alisema, “Tumefurahishwa sana na ushindi wa bwana Robert na tunapenda kumshukuru kwa kushiriki na tunaamini aliifurahia bia ya Serengeti Premium ambayo imemletea furaha ya kipekee siku ya leo.
Rodney pia alitumia fursa hiyo kuwashukuru washiriki wote kwa kutumia muda wao wa thamani katika promosheni hii  na kuwapa moyo wale ambao hawakubahatika kushinda mtoko wa mbugani, Bajaj au bia za bure kutokata tamaa na kushiriki tena nyakati zijazo kwani SBL imekuwa mstari wa mbele katika kurudisha kiasi cha faida waliyopata kwa wateja wake. Aliongeza kuwa wateja wakae mkao wa kula kwani kuna kitu kikubwa kinaandaliwa kwa ajili yao.
Wakati kampeni hii iliyodumu takribani miezi minne inafikia tamati, SBL imetoa shukrani za pekee kwa wateja wake wa Serengeti Premium Lager baada ya kushuhudia  washiriki zaidi ya milioni moja wakijaribu bahati zao na kuifanya promosheni ya “Tutoke na Serengeti” kuwa yenye mafanikio  kutokana na muitikio mkubwa na uelewa kutoka kwa wananchi.
Kampeni imewazawadia wateja mbalimbali fursa ya kutembelea mbuga ya wanyama ya Serengeti wakati wengine wakiondoka na zawadi murua kama vile Limo Bajaj ambazo kwa kiasi kikubwa zitabadilisha maisha yao. Kulikuwa pia na fedha taslim za kila wiki, bia za bure, na punguzo la Tshs300 katika kila bia ya Serengeti Premium.
Promosheni hii ya nchi nzima pia ilipata ushirikiano wa hali ya juu kutoka kwa B-Pesa, wataalamu wa teknolojia mpya ya usambazaji fedha waliochangia Limo Bajaj sita kwa washindi mbalimbali. Pia walihusika na usambazaji wa fedha kwa washindi nchi nzima katika kipindi chote cha miezi mine ya kampeni.

NUHU MZIWANDA KINGEREZA CHAMPIGA CHENGA ACHAPIA KINGEREZA MARA TATU MFULULIZO

$
0
0





Sasa ndugu yangu NUHU umezidishaaa khah...Tutamwambia Shishi aache kukupiga TUKUPIGE SISI maana unatuvurugaaaa kwakweli halafu HUKOMI,unaangusha 1 baada ya lingine kudaadeki... Ipo siku utaumwa Kichwa halafu utaandika "Iam going to table the tablets of head pain" (Naenda kumeza dawa za maumivu ya kichwa) WALLAH TUTAKUPIGA!

Kauli Mpya ya Zitto Kabwe Kuhusu Hatma Yake ya Urais na Ubunge Hii Hapa

$
0
0
“Wakati wa sakata la Escrow bungeni, kuna mjumbe mmoja wa PAC aliitwa na vinara wa watuhumiwa wa Escrow na kutakiwa kusema uongo bungeni kuhusu mimi kwa ahadi ya kupewa donge nono, mjumbe huyo alikataa, na hapo ndipo vinara hao wa Escrow wakaapa kutenga Shilingi Milion 500 kwa kila jimbo la kila mjumbe wa PAC kuhakikisha kuwa wajumbe hao wote hawarudi bungeni.

Kwahiyo nahisi kuwa hiki kilichonitokea sasa ni sehemu ya mkakati huo maana sakata la escrow limegusa wengi, hadi majaji wamo.”
“Kama Katiba ingebadilishwa kabla ya uchaguzi mkuu 2015 na ikaruhusu mgombea urais mwenye umri chini ya miaka 40, ningegombea urais, nahitaji kuongoza nchi, kwa ubunge imetosha, lakini kwa kuwa haiwezekani, nitagombea ubunge lakini si Kigoma Kaskazini, nitatafuta jimbo linguine la kugombea ili nao nikawatumikie, Kigoma Kaskazini nimeshafanya kila kitu, sitakuwa na jipya”
Hajasema atagombea kupitia chama gani,

Je, wewe ungependa agombee kwa chama gani, jimbo gani na nini maoni yako kuhusu kauli hii?

Picha, Wanawake 5 wanaoongoza kwa mvuto bongo movie.

$
0
0
List ya wanawake wenye mvuto zaidi kwenye tasnia ya bongo movie iliyotolewa na mtandao wa bongo movie ndio hii. Namba moja imechukuliwa na mwigizaje asiyeweka mambo yake wazi Welu Sengo.
  1. Anaitwa Welu Sengo
Welu sengo
2. Yobnesh Yusuph Aka Batuli
Batuli
3. Tatu imechukuliwa na Wema Sepetu
wema-sepetu-miss-tz-2006
4.Elizabeth Michael aka Lulu
lulu
5. Irene Uwoya
irene_uwoya
Unamtazamo gani juu ya hii list iliyotolewa na mtandao wa Bongo Movie ?

Diamond Platnumz Hana Njaa Akataa Show ya Tshs Milioni 54 Uganda?

$
0
0
Diamond Platnumz
Diamond Platnumz hana njaa na ndio maana alizikataa dola 30,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 54 za Tanzania kufanya show nchini Uganda?

Hiyo ni kwa mujibu wa rapper maarufu wa Uganda, Atlas Da African aliyekuwepo nchini wiki hii, baada ya Diamond kuwa chanzo cha kuijaza club Guvnor kwenye All White CIROC Party iliyoandaliwa na mpenzi wake Zari the Bosslady December 18 mwaka jana, makampuni kadhaa yalijitokeza kumtaka msanii huyo afanye show yake mwenyewe.

Kwa mujibu wa Atlas, kampuni moja ilimpa ofa hiyo Diamond ambaye hata hivyo alikataa.

Akiongea kwenye kipindi cha Clouds E cha Clouds TV, Atlas alidai kuwa hiyo ilionesha ni kiasi gani Diamond ana msimamo kwakuwa anajua kwa sasa kila mtu anamfahamu nchini humo na anaweza kupata fedha nyingi zaidi ya hizo.

Hata hivyo meneja wa Diamond, Salam amekanusha msanii wake kukataa kiasi hicho cha fedha.

“Hakuna show iliyokataliwa ila tulikuwa tunaongea na middle man sasa sijui yeye aliwaambia waandaji kiasi gani, plus walikuwa wanataka club appearance na show the next day kwa bei ya show peke yake kwahiyo show haikukataliwa tulikubaliana bei lakini hawakurudi tena,” Salam ameiambia Bongo5.

Kamikaze Afunguka Kuhusu Kumnyang'anya Demu Bob Junior na Video ya Malavidavi Chumbani

$
0
0
Mwanamuziki Kamikaze Amefunguka kuhusu Kumnyang'anya Demu Bob Junior na Video iliyovuja akiwa na Mrembo Sabby Chumbani Huku Mrembo huyo ambae ni Demu wa Bob Junior Akijinadi Kwa kumwita Kamikaze Baby na kusema wako vacation:

 Angalia Hapa Chini Udaku TV Inakuletea Umbea Huo Wote:
Viewing all 3623 articles
Browse latest View live