Quantcast
Channel: BongoClan Tanzania™
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3623

MIKE TYSON SASA ATANGAZWA RASMI KUA KAFIRISIKA, ALIWAHI KUTUMIA $400 MILIONI KWA MWAKA. SOMA HAPA

$
0
0

TUMIA pesa kwa akili. Unajua kwa nini? Mtazame Mike Tyson, utapata jibu. Bondia huyo bingwa wa dunia wa masumbwi ya uzito wa juu, ameandika historia ya aina yake ya kimaisha katika kipindi hiki cha uhai wake.
Achana na kesi ya kufungwa jela kwa madai ya kubaka, au tukio la kumng’ata sikio mpinzani wake ulingoni, Evander Holyfield, Tyson, bondia aliyekuwa tishio kwenye ngumi za kulipwa na kupiga pesa za maana sasa kipato chake ni Dola 1 Milioni tu.
Wakati anang’ara ulingoni, bondia huyo alitajwa kuwa na kipato kinachofikia Dola 300 milioni, lakini kwa sasa anaripotiwa kubaki na Dola 1 milioni ndiyo utajiri wake aliobaki nao.
Makuzi yake
Tyson alizaliwa Juni 30, 1966 huko Brooklyn New York, Marekani kwenye eneo hatari sana. Akiwa na umri wa miaka 13 tu, Tyson alikuwa tayari amekamatwa na polisi mara 38 na alikuwa akifanya matukio ya hatari sana.
Utukutu wake ulizidi zaidi alipojiunga na shule ya wavulana ya Tryon, mahali ambako alijifunza ngumi. Bobby Stewart, ndiye aliyeanza kumfundisha ngumi bondia huyo kabla ya kumkabidhi kwa kocha Cus D’Amato.
Cus D’Amato aliendelea kumnoa Tyson hadi hapo alipoanza kumsimamia kisheria kutokana na mama yake Tyson kufariki dunia wakati huo bondia huyo akiwa na umri wa miaka 16.
Jinsi alivyopiga pesa
Pesa kwa Mike Tyson zilipatikana kutokana na umahiri wake ulingoni. Ushindi kwenye mapambano yake ulimfanya kuwa bondia mwenye pesa na kupata udhamini mnono. Alikuwa akilipwa hadi Dola 5 milioni kwa pambano moja.
Ushindi wake wa kwanza ulikuwa kwenye mashindano ya Olimpiki aliposhinda medali ya fedha mwaka 1982.
Machi 6, 1985, Tyson alianza kupigana ngumi za kulipwa wakati alipopigana na Hector Mercedes. Mambo yalikuwa mazuri na kushinda mapambano 26 kati ya 28 na hapo alijikusanyia umarufu mkubwa.
Mwaka 1985, Tyson alipata pigo baada ya kumpoteza Cus D’Amato, mtu muhimu zaidi kwake na hapo pesa zilianza kuwa ngumu. Februari 16, 1986, Tyson kwa mara ya kwanza pambano lake lilionyeshwa kwenye televisheni alipomtwanga Jesse Ferguson.
Kwenye umri wa miaka 20 tu, Tyson alikuwa bondia kijana zaidi kunyakua ubingwa wa dunia, aliwachapa James Smith, Pinklon Thomas na Tony Tucker na kutambulika kuwa bondia bora Marekani.
Jambo hilo lilimpatia pesa zaidi baada ya kuwekwa kwenye michezo ya kompyuta mwaka 1987, ambapo video yake ya Nintendo iliyotambulika kama ‘Mike Tyson’s Punch-Out!!!’ iliingizwa sokoni.
Jinsi alivyofilisika
Mwaka 1988, mambo yalianza kumgeuka Tyson. Matumizi mabaya ya pesa yalichangia kufilisika kwake. Kwenye kipindi cha ubora wake, Tyson aliingiza pesa hadi Dola 400 milioni, lakini kabla hata ya kufikisha umri wa miaka 39, mwaka 2004, Tyson alikuwa akiishi kwenye madeni yanayofikia Dola 38 milioni.
Enzi zake, Tyson alikuwa ameajiri wafanyakazi 200, wakiwamo walinzi binafsi, wapishi na watunza bustani.
Tyson alitumia karibu Dola 4.5 milioni kwenye magari na pikipiki, Dola 3.4 milioni kwenye mavazi na mapambo, Dola 7.8 milioni gharama tu za mambo binafsi, Dola 125,000 malipo ya kocha kwa mwaka, Dola 2 milioni kurekebisha bafu la mkewe wa kwanza, mwigizaji Robin Givens, Dola 410,000 zilitumika kwenye kusherehekea kuzaliwa na Dola 230,000 kwenye gharama za huduma ya simu kwa miaka mitatu kutoka 1995 hadi 1998. Kwenye mahojiano yake ya hivi karibuni, Tyson alikiri kutumia hadi Dola 500 milioni katika miaka ya 1980.
Kufilisika kulimchanganya Tyson na kumwambia mkewe wa pili, Monica Turner kabla ya kumtaliki kwamba alikuwa ameathirika kwa Ukimwi jambo ambalo halikuwa kweli.
Alipokuwa kifungoni, Tyson alikuwa akifanya ngono na wanawake waliokuwa wakimtembelea gerezani, akiwamo mrembo mshauri wa masuala ya matumizi ya dawa za kulevya, ambaye alimlipa Dola 10,000 kwa huduma hiyo. Pombe pia zilimfanya kupoteza mkoba uliokuwa na Dola 1 milioni.
credit : MWANANCHI

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3623

Trending Articles