Quantcast
Channel: BongoClan Tanzania™
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3623

DULLY SYKES AMTETEA DIAMOND KUHUSU TUHUMA ZA KUTEGEMEA MGANGA WAKE KUPTA MAFANIKIO ALIYOKUWA NAYO SASA..!

$
0
0


Jina la Diamond Platinumz mtoto wa Tandale mwenye historia ya kuishi maisha ya ukata, sasa hivi ni moja kati ya majina makubwa kimuziki barani Afrika huku akishiriki kwenye project kubwa kama One Campaign iliyoongozwa na D’Banj huku akipewa mashavu na wasanii wakubwa wa Afrika Magharibi.

Dully Sykes ameuambia mtandao wa Times Fm moja kati ya sababu ambazo zinambeba mwimbaji huyo na kumpeleka kwenye level ya juu ya mafanikio kuwa ni kiu kubwa aliyonayo inayomfanya afanye kazi usiku na mchana huku akiwasumbua maproducer bila kusubiri wamuite studio.

“Wasimuone Diamond anafanya vizuri, Diamond anafika mbali wakafikiria Diamond anafanya kazi kwa kumsubiria hadi producer amuite studio, no sio kweli. Diamond anashinda usiku kila siku studio.” Amesema Dully Sykes.

Dully ameeleza kuwa hata yeye pia hukesha studio akifanya kazi na ndio sababu inayomfanya aendelee kufanya vizuri tangu alipoanza muziki bila kupotea na kwamba wasanii wengi wasiofanya hivyo huishia kuporomoka na kudai kuwa walioko juu wanafanya uchawi.

Mwimbaji huyo ambaye ni mmiliki wa studio ya 4.12 ameongeza kuwa akili ya kuwekeza kwenye vitega uchumi pindi uwapo juu ni moja kati ya sababu zinazomsaidia msanii kuendelea kuwa juu kwa muda mrefu.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 3623

Trending Articles